• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Kondoa Town Council
Kondoa Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Kondoa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Mipango ,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu sekondari
      • Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
      • Idara ya Usafi na Mazingira
      • Divisheni
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Miundombinu Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Viwanda Bishara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Usimamizi na Utawala wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugi na Uvuvi
    • Kitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Teknolojia,Habari,Mawasiliano na uhusiano
      • Kitengo cha Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DKT. MAHENGE AKUTANA NA WAKUU WA VYUO VIKUU NA ELIMY YA JUU VYA DODOMA

Tarehe iliyowekwa: November 7th, 2017

 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge katikati ya wiki amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Vyuo Vikuu, Elimu ya Juu na Ufundi Stadi Mkoani Dodoma na kwa pamoja wamejadili masuala mbalimbali ya Maendeleo ya Mkoa wa Dodoma Makao Makuu ya Nchi.

Katika Mkutano huo Dkt. Mahenge amepongeza mchango wa Vyuo Vikuu, Elimu ya Juu na Ufundi Stadi Mkoani Dodoma na kubainisha kuwa ipo haja ya kukuza zaidi ushirikiano kati ya Serikali ya Mkoa na Taasisi hizo za Elimu ambapo amezitaka zijikite katika kufanya tafiti za kitalaamu juu ya namna ya kutatua changamoto za wananchi na kuboresha zaidi shughuli mbalimbali za uchumi, uzalishaji na uwekezaji kwa lengo la kuufanya Mkoa wa Dodoma uwe na kasi kubwa ya maendeleo zaidi ya ilivyo sasa.

Ametaja maeneo makuu ya ushirikiano ni pamoja na eneo zima la ujio wa Serikali Mkoani Dodoma Makao Makuu ya nchi na kuzitaka Taasisi hizo za Elimu kusaidia kuwaandaa wananchi wa Dodoma juu ya namna bora za kuchangamkia fursa hiyo ya ujio na kuainisha bayana maeneo ya fursa zinazoambatana na ujio wa Serikali.

Aidha, ametaja eneo jingine muhimu linalohitaji mchango mkubwa wa Taasisi hizo za Elimu ni Eneo la kuelekea Tanzania ya Viwanda ambapo Mkoa unahitaji kuandaa nguvu kazi ya kutosha na yenye ujuzi kwenye fani mbalimbali zinazohitajika kwenye viwanda vilivyopo na vinavyoendelea kujengwa na kutaja Taasisi kama ya VETA inaweza kutoa mchango mkubwa kuwaandaa vijana ili watafutiwe mitaji waweze kujiajiri kwa kuanzisha viwanda vidogo, vya kati na hatimaye vikubwa.

Amebainisha kuwa Mkoa pia unahitaji ushirikiano na Taasisi hizo kwenye eneo la Elimu hususani suala la kuinua kiwango cha ufaulu kwa kusaidia ufundishaji kwenye shule za Dodoma na mafunzo kwa walimu wa Mkoa wa Dodoma. Amesema kwa hali ya sasa bado kiwango cha Ufaulu cha Mkoa wa Dodoma hakiridhishi akitolea mfano kuwa wastani wa kiwango cha ufaulu cha Mkoa wa Dodoma kwenye mtihani wa kumaliza Elimu ya msingi kwa mwaka huu 2017 ni asilimia 63.68% hivyo kuufanya Mkoa kushika nafasi ya 24 kati ya mikoa 26.

Dkt. Mahenge pia ameziomba Taasisi hizo za Elimu kuona namna ya kubuni programu mbalimbali za utunzanji Mazingira ya Mkoa wa Dodoma kwa kuwashirikisha wanafunzi wake katika utekelezaji kama moja ya njia ya kufanyia kazi kwa vitendo elimu wanayopewa darasani na kubainisha kuwa utunzaji wa mazingira utapunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na kuboresha hali ya hewa.

Akipongeza jitihada za Serikali ya awamu ya Tano Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo vijijini (IRDP) Profesa Hozen Mayaya amemweleza Mkuu wa Mkoa kuwa, Chuo chake kitajikita zaidi katika suala zima la Tafiti na kuziwezesha Halmashauri za Wilaya za Mkoa wa Dodoma katika uandaaji wa mipango ya Maendeleo ambayo itagusa hadi wananchi kwenye ngazi za msingi.

Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA) Dodoma Ndugu Ramadhani Mataka amesema tayari chuo chake kilishaanza programu za kuwaandaa vijana kwa kuwapa ujuzi kwenye fani mbalimbali ambapo tayari Vijana zaidi ya 800 waliokuwa kwenye soko la uzalishaji mtaani kwenye fani mbalimbali walipatiwa mafunzo rasmi na kusajiliwa, Amesema kuwa programu hiyo itaendelea ili kuwafikia vijana wengi zaidi hapa Mkoani Dodoma.

Mkurugenzi wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Kampasi ya Dodoma Ndugu Omary Ally amesema kuwa tayari chuo chake kilishaanza utaratibu wa kuandaa makongamano ya Biashara, Uchumi na Uwekezaji yakiangazia fursa mbalimbali zinazokuja na ujio wa Serikali Mkoani Dodoma na kubainisha kuwa mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka huu kongamano lingine litafanyika lenye lengo la kuangazia Dhana ya Tanzania ya Viwanda kwa maendeleo endelevu ya kiuchumi ambapo wataalamu wa chuo chake watawasilisha matokeo ya tafiti mbalimbali walizozifanya.

Pia amesema ili kusaidia eneo la elimu na kiwango cha ufaulu Mkoani Dodoma chuo chake kitaandaa programu za kutoa wataalamu wake na wanafunzi wake wakati wa mazoezi ya vitendo kwenda kufundisha kwenye shule za Dodoma, lakini pia wataandaa programu maalumu za kuwajengea uwezo walimu wa Dodoma na kuwa kwa sasa tayari chuo hicho kimeanzisha kozi ya shahada ya kwanza ya ualimu wa masomo ya biashara.

Matangazo

  • Tangazo la mikopo inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu February 21, 2025
  • Matokeo ya kidato cha nne 2024 shule za Sekondari Kondoa Mji January 23, 2025
  • Tangazo la kushiriki mazoezi ya kila Jumamosi ya pili kila mwezi January 02, 2025
  • Tangazo la umilikishwaji viwanja January 02, 2025
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • Mkurugenzi Majaliwa aagiza miradi kukamilika ifikapo Mei 31

    May 08, 2025
  • ALAT mkoa wa Dodoma yatembelea miradi ya maendeleo Kondoa Mji

    May 03, 2025
  • Baraza la Madiwani lajivunia mafanikio kipindi cha miaka mitano

    April 30, 2025
  • Baraza la kazi robo ya tatu lafanyika Kondoa Mji Ushirikiano ukisisitizwa

    April 29, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Matukio ya Mwenge wa Uhuru Kondoa Mji 2025
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mpango Mkakati
  • Maktaba ya Picha
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Sheria ndogo
  • Ripoti Mbalimbali
  • Fomu Mbalimbali
  • Miradi Inayoendelea

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Kwapakacha

    Anuani ya Posta: S.L.P 711

    Simu ya Mezani: +255 712264912

    Simu ya Mkononi: +255 712264912

    Barua Pepe: td@kondoatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Kondoa - Haki Zote Zimehifadhiwa