• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Kondoa Town Council
Kondoa Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Kondoa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Mipango ,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu sekondari
      • Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
      • Idara ya Usafi na Mazingira
      • Divisheni
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Miundombinu Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Viwanda Bishara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Usimamizi na Utawala wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugi na Uvuvi
    • Kitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Teknolojia,Habari,Mawasiliano na uhusiano
      • Kitengo cha Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kondoa Mji Yapongezwa Kuzindua Baraza la Wafanyakazi

Tarehe iliyowekwa: January 25th, 2019

Halmashauri ya Mji wa Kondoa imepongezwa kwa kufanya uzinduzi wa baraza la wafanyakazi ikiwa ni halmashauri ya pili katika mkoa wa Dodoma kufanya hivyo.

Pongezi hizo zilitolewa na Katibu Tawala wa Wilaya Andrea Mwani wakati akizindua baraza hilo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya uzinduzi uliofanyika katika ukumbi wa Kondoa Irangi Kondoa Mjini.

Alisema kuwa uwepo wa baraza hilo ikawe chombo cha kusema katika kufikisha matakwa ya watumishi na kuimarisha ushirikiano na mwajili na kuwa anauhakika katika baraza hilo wajumbe watawasilisha wanayoona yatafaa katika kushirikiana na mwajiri kutatua changamoto za kazini.

”Mnaweza mkaona katika uongozi huu wa awamu ya tano jinsi Mheshimiwa Rais anavyofanya mabadiliko ya kuiendeleza nchi na wakuyafanya haya ni sisi wafanyakazi hivyo kila mmoja awajibike katika eneo lake na kujitathmini ili tuendane na upepo uliopo.”Alisema Mwani

Aidha alisisitiza wafanyakazi kufanyakazi na kutimiza majukumu yao walioajiliwa nayo kwa asilimia zote pamoja na melekezo wanayopewa kwani kwa kufanya hivyo wanamsaidia Mheshimiwa Rais, Mkuu wa Wilaya, Halmashauri na wananchi wanaowahudumia.

Aidha kwa upande wake Mkurugenzi wa Mji Kondoa Msoleni Dakawa alisema kuwa baraza limeanzishwa baada ya kuona umuhimu wa wafanyakazi kwa kuwa katika serikali mfanyakazi ndio mzalishaji na mtekelezaji wa maagizo na ahadi zinazotolewa na serikali.

“Niombe kwa wakati mwingine kwa umoja huu tuliouonyesha na vyama vya wafanyakazi tuendelee nao iwe wakati wa shida na raha kwani lengo ni kuhakikisha mambo yanaenda nai tuna wajibu wa kupambana kama anavyofanya Mheshimiwa Rais lengo likiwa kuwahudumia wananchi na kuwapatia haki zao watumishi.” Alisisitiza Dakawa

Naye mwakilishi wa vyama vya wafanyakazi  ambaye ni Katibu wa TUGHE mkoa wa Dodoma Bwana Mchenya John alisema kuwa baraza la wafanyakazi ni chombo muhimu cha maamuzi kwa halmashauri na kuwataka wajumbe wa baraza kuacha uoga na kujadili mambo yatakayowasaidia kuendesha halmashauri na maslahi ya watumishi.

“Namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kulitolea maamuzi suala la kikokotoo kwani liliwakatisha taama sana wafanyakazi na nilishakuja hapa mwaka jana nikapata fursa ya kuongea na wafanyakazi na nashukuru walinielewa na kuwa watulivu wakati wote wa mpito hadi Mheshimiwa Rais alipolitolea maamuzi.”Alimaliza Bwana Mchenya.                                                                                                                                                                                                                                                                                                          

Matangazo

  • Tangazo la mikopo inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu February 21, 2025
  • Matokeo ya kidato cha nne 2024 shule za Sekondari Kondoa Mji January 23, 2025
  • Tangazo la kushiriki mazoezi ya kila Jumamosi ya pili kila mwezi January 02, 2025
  • Tangazo la umilikishwaji viwanja January 02, 2025
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • SHULE BORA yawapatia mafunzo ya tathmini Walimu 66 wa Kondoa Mji

    May 26, 2025
  • "Vitengo vya Mawasiliano Serikalini viimarishwe"

    May 24, 2025
  • Maafisa Habari hakikisheni wananchi wanapata habari sahihi

    May 23, 2025
  • Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari la awali ngazi ya kata yatolewa kwa Watendaji Kondoa Mji

    May 14, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Matukio ya Mwenge wa Uhuru Kondoa Mji 2025
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mpango Mkakati
  • Maktaba ya Picha
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Sheria ndogo
  • Ripoti Mbalimbali
  • Fomu Mbalimbali
  • Miradi Inayoendelea

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Kwapakacha

    Anuani ya Posta: S.L.P 711

    Simu ya Mezani: +255 712264912

    Simu ya Mkononi: +255 712264912

    Barua Pepe: td@kondoatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Kondoa - Haki Zote Zimehifadhiwa