• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Kondoa Town Council
Kondoa Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Kondoa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Mipango ,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu sekondari
      • Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
      • Idara ya Usafi na Mazingira
      • Divisheni
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Miundombinu Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Viwanda Bishara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Usimamizi na Utawala wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugi na Uvuvi
    • Kitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Teknolojia,Habari,Mawasiliano na uhusiano
      • Kitengo cha Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

"Sekta ya Habari ipo mikono salama"- Waziri Nape

Tarehe iliyowekwa: June 19th, 2024

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb) amewahakikishia wadau wa sekta ya habari kuwa sekta ipo kwenye mikono salama.

Waziri Nape ametoa ahadi hiyo tarehe 19 Juni, 2024 wakati akifunga Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari lililofanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 18 hadi 19 Juni, 2024, kwenye ukumbi wa mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Mhe. Nnauye ameeleza kuwa Kongamano hilo limewaunganisha wadau wote wa sekta ya habari na limechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza ukuaji wa sekta hiyo.

“Wanahabari niwahakikishie kuwa Sekta ya Habari ipo mikono salama. Tuweke utamaduni wa kujadiliana vitu vitakavyoleta maendeleo katika nchi yetu. Kwa siku mbili tulizokuwa hapa tumejenga misingi bora zaidi, tumepata fursa ya kujadiliana mambo mbalimbali”.

Alifafanua kuwa sekta ya habari ni muhimu katika kuleta mageuzi ya kiuchumi, kijamii na hata kisiasa, hivyo wanahabari wakiamua, wana uwezo wa kurahisisha na kuchochea maendeleo ya Taifa kwa kasi zaidi.

Pia Waziri Nape ameishukuru Kamati aliyoiundwa kutathmini hali ya uchumi wa vyombo vya habari ikiongozwa na Bw. Tido Mhando kwa kazi nzuri waliyoifanya na kuahidi kuwa yote yaliyowasilishwa kwenye ripoti yao yatafanyiwa kazi.

“Niombe ripoti hii iwe chanzo cha mijadala zaidi. Ninaamini ripoti hii haiwezi kuwa muarobaini wa matatizo ya wanahabari lakini ni mwanzo mzuri kuelekea mabadiliko tunayoyatamani. Niwaombe wadau wengine walioguswa na ripoti hii waangalie yanayowahusu na wayafanyie kazi” amesisitiza Mhe. Nnauye.

Wakati huo huo, Mhe. Nnauye amewaeleza wadau wa sekta ya habari kuwa mambo yote waliyokubaliana yatafanyiwa kazi na yanayowezekana kufanyiwa kazi kwa sasa yatafanyiwa na yasiyowezekana kwa sasa yatafanyiwa kazi kwa wakati sahihi.

“Wanahabari wenzangu niwahakikishie mimi ni muumini wa uhuru wa vyombo vya habari. Mada zilizowasilishwa na maazimio tuliyojiwekea yakawe chachu ya maendeleo ya sekta yetu. Nataka niwahakikishie wanahabari nyinyi ni wadau na si washindani wa Serikali” amesema Mhe. Nnauye.

Kongamano la Pili la Maendeleo ya Sekta ya Habari limehusisha wahariri wa vyombo vya habari, waandishi wa habari na maafisa habari wa Serikali, likibeba kauli mbiu ya ‘Jenga mustakabali endelevu kwenye sekta ya habari katika zama za kidijiti’.



Matangazo

  • Tangazo la mikopo inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu February 21, 2025
  • Matokeo ya kidato cha nne 2024 shule za Sekondari Kondoa Mji January 23, 2025
  • Tangazo la kushiriki mazoezi ya kila Jumamosi ya pili kila mwezi January 02, 2025
  • Tangazo la umilikishwaji viwanja January 02, 2025
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • SHULE BORA yawapatia mafunzo ya tathmini Walimu 66 wa Kondoa Mji

    May 26, 2025
  • "Vitengo vya Mawasiliano Serikalini viimarishwe"

    May 24, 2025
  • Maafisa Habari hakikisheni wananchi wanapata habari sahihi

    May 23, 2025
  • Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari la awali ngazi ya kata yatolewa kwa Watendaji Kondoa Mji

    May 14, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Matukio ya Mwenge wa Uhuru Kondoa Mji 2025
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mpango Mkakati
  • Maktaba ya Picha
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Sheria ndogo
  • Ripoti Mbalimbali
  • Fomu Mbalimbali
  • Miradi Inayoendelea

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Kwapakacha

    Anuani ya Posta: S.L.P 711

    Simu ya Mezani: +255 712264912

    Simu ya Mkononi: +255 712264912

    Barua Pepe: td@kondoatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Kondoa - Haki Zote Zimehifadhiwa