• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Kondoa Town Council
Kondoa Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Kondoa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Mipango ,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu sekondari
      • Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
      • Idara ya Usafi na Mazingira
      • Divisheni
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Miundombinu Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Viwanda Bishara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Usimamizi na Utawala wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugi na Uvuvi
    • Kitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Teknolojia,Habari,Mawasiliano na uhusiano
      • Kitengo cha Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

"Simamieni miradi ikamilike kwa wakati" - DC Nyangasa

Tarehe iliyowekwa: August 3rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Fatma Nyangasa amewataka Wakuu wa Idara wa Halmashauri ya Mji Kondoa kusimamia miradi iliyochini ya idara zao ili ikamilike kwa wakati uliopangwa na ubora.

Ameyasema hayo wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi aliyoifanya ili kujionea utekelezaji wake ambapo aliongozana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kondoa, Mkurugenzi wa Halmashauri na wakuu wa Idara.

Akiongea katika mradi wa ujenzi wa madarasa, ukarabati wa maabara na ujenzi wa vyoo Shule ya Sekondari Serya Mhe. Fatma amewataka Idara ya Elimu kumsimamia kwa karibu fundi anayetekeleza mradi huo kwa kuhakikisha kuwa anakamilisha ndani ya mwezi huu.

"Fundi ongeza mafundi wa kutosha hapa tupo nje ya muda sintakuelewa kabisa ikifika tarehe 15 utukabidhi mradi huu mimi nitakuja tarehe 10 kuangalia ulipofikia sasa nisikute hizi hadithi za sasa"amesisitiza Mhe. Fatma

Hata hivyo amewataka Wahandisi kufika mara kwa mara katika miradi na kutoa maelekezo stahiki kwa mafundi ili wajenge miradi katika viwango vinavyotakiwa ikiwa ni pamoja na kusaini katika vitabu vya eneo la miradi.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kondoa Ndg. Said Majaliwa amemshukuru Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya kwa kupitia miradi na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote aliyoyatoa kwani amekuwa akipita na kuongea na mafundi hao mara kwa mara.

"Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya mimi huwa nakuja kwenye miradi hii na kutoa maelekezo hata paha Serya niliongea na fundi akanieleza changamoto yake nikaifanyia kazi na nikamwambia aongeze mafundi lakini hajafanya hivyo ila nakuahidi tutasimamia na itakamilika kwa wakati"amesema Mkurugenzi Majaliwa

Mkuu wa Wilaya amefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya Stendi ya Bicha, eneo la maegesho ya malori, Zahanati ya Mulua, ujenzi Serya Sekondari na Kituo cha Afya Serya ambapo aliambatana na Katibu Tawala Wilaya Ndg. Christina Kalekezi.

Matangazo

  • Tangazo la mikopo inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu February 21, 2025
  • Matokeo ya kidato cha nne 2024 shule za Sekondari Kondoa Mji January 23, 2025
  • Tangazo la kushiriki mazoezi ya kila Jumamosi ya pili kila mwezi January 02, 2025
  • Tangazo la umilikishwaji viwanja January 02, 2025
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • ALAT mkoa wa Dodoma yatembelea miradi ya maendeleo Kondoa Mji

    May 03, 2025
  • Baraza la Madiwani lajivunia mafanikio kipindi cha miaka mitano

    April 30, 2025
  • Baraza la kazi robo ya tatu lafanyika Kondoa Mji Ushirikiano ukisisitizwa

    April 29, 2025
  • Wasira aelezea faida za Muungano kwa wananchi wa Kondoa

    April 26, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Matukio ya Mwenge wa Uhuru Kondoa Mji 2025
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mpango Mkakati
  • Maktaba ya Picha
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Sheria ndogo
  • Ripoti Mbalimbali
  • Fomu Mbalimbali
  • Miradi Inayoendelea

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Kwapakacha

    Anuani ya Posta: S.L.P 711

    Simu ya Mezani: +255 712264912

    Simu ya Mkononi: +255 712264912

    Barua Pepe: td@kondoatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Kondoa - Haki Zote Zimehifadhiwa