• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Kondoa Town Council
Kondoa Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Kondoa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Mipango ,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu sekondari
      • Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
      • Idara ya Usafi na Mazingira
      • Divisheni
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Miundombinu Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Viwanda Bishara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Usimamizi na Utawala wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugi na Uvuvi
    • Kitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Teknolojia,Habari,Mawasiliano na uhusiano
      • Kitengo cha Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Uwazi wasisitizwa kwenye utekelezaji wa miradi

Tarehe iliyowekwa: November 8th, 2023

Ushirikiano na uwazi vimetakiwa kuzingatiwa wakati wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyopata fedha zaidi ya shilingi bilioni 1.1 katika robo ya kwanza ili fedha zilizoletwa zitumike vizuri na kusaidia katika kutatua changamoto zingine.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kondoa Mhe. Mohamed Kiberenge wakati wa kikao cha baraza la Waheshimiwa madiwani robo ya kwanza kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji Kondoa hivi karibuni.

“Waheshimiwa Madiwani tunapaswa kuwa karibu na miradi tusiwaachie wataalam peke yao twende tukasimamie ili miradi ikamilike kwa wakati na ubora unaotakiwa na si lazima fedha iliyoletwa iishe yote na hili linawezekana tukisimamia vizuri,”amesema Mhe. Kiberenge

Ameongeza kuwa mahitaji halisi yajulikane mapema ili kujua kiasi cha fedha kitakachotumika na ikibaki itasaidia kwenye kutatua changamoto zingine na kwa kutumia fedha kinyume ni kutowatendea haki wananchi wengine wenye mahitaji.

“Madiwani ndio wenyeviti wa maendeleo wa kata hatutegemei mradi ulioletewa fedha usikamilike na ambao hadi sasa kamati hazijaundwa mkaziunde ili TAKUKURU pia wanaopita huko wakatoe elimu kwa kamati hizo na penye changamoto msisite kuomba ushauri ili mambo yasikwame,”amesisitiza Mhe. Kiberenge

Akiongea Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Dkt. Khamis Mkanachi amewataka maafisa tarafa kwenda kushirikiana na watendaji wengine katika maeneo yao ili kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwani kwa kuongeza nguvu na kufanya kazi kwa pamoja usimamizi utakuwa mzuri na miradi itakamilika kwa wakati ikiwemo miradi yenye afya ambayo ndio imeonekana kuwa na changamoto zaidi.

“Tumefanya kazi ya usafi mitaani lengo lilikuwa kuwafanya wananchi waelewe dhana ya usafi sababu tumegundua wananchi wengi wanafanya usafi katika nyumba zao na si maeneo ya wazi au mifereji hawafanyi hivyo afisa mazingira hakikisha unasimamia usafi wa mji na chukua hatua za kisheria kwa wote wanaochafua mazingira na kufanya agenda ya afya kuwa ni ya kila siku ikiwemo kupanda miti na kuitunza,”amesema Dkt. Mkanachi

Akitoa taarifa ya mapokezi ya fedha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kondoa Ndg. Paul Sweya amesema Halmashauri imepokea shilingi bilioni 1.1 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya madarasa, umaliziaji wa zahanati za Mulua na Choka na ununuzi wa vifaa tiba kwa ajili ya sehemu za kutolwa huduma za afya kwa kipindi cha robo ya kwanza.

“Naomba waheshimiwa madiwani mkatusaidie kuhamasisha wananchi wakachangie nguvu zao na ulinzi wa miundombinu hiyo pamoja na vifaa vya ujenzi sababu ni kwa manufaa yao lakini pia  kuendana na   kasi ya serikali na mapenzi ya serikali kwa wananchi wake,”amesema Mkurugenzi Sweya

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kondoa Ndg. Hija Sulu amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha zote hizo kwa kipindi cha robo ya kwanza na kuwataka watendaji kuacha tabia ya kufanya kazi kwa kwa mazoea zaidi ni kushirikishana palipo na changamoto ili zifanyiwe kazi.

Baraza la Waheshimiwa Madiwani robo ya kwanza limefanyika ambapo limehudhuriwa na Mkuu wa Wilaya na kamati ya Usalama, viongozi wa taasis za serikali zilizopo Kondoa, Wakuu wa Idara, Wananchi na viongozi wa Chama cha Mapinduzi.

Matangazo

  • Tangazo la mikopo inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu February 21, 2025
  • Matokeo ya kidato cha nne 2024 shule za Sekondari Kondoa Mji January 23, 2025
  • Tangazo la kushiriki mazoezi ya kila Jumamosi ya pili kila mwezi January 02, 2025
  • Tangazo la umilikishwaji viwanja January 02, 2025
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • SHULE BORA yawapatia mafunzo ya tathmini Walimu 66 wa Kondoa Mji

    May 26, 2025
  • "Vitengo vya Mawasiliano Serikalini viimarishwe"

    May 24, 2025
  • Maafisa Habari hakikisheni wananchi wanapata habari sahihi

    May 23, 2025
  • Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari la awali ngazi ya kata yatolewa kwa Watendaji Kondoa Mji

    May 14, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Matukio ya Mwenge wa Uhuru Kondoa Mji 2025
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mpango Mkakati
  • Maktaba ya Picha
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Sheria ndogo
  • Ripoti Mbalimbali
  • Fomu Mbalimbali
  • Miradi Inayoendelea

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Kwapakacha

    Anuani ya Posta: S.L.P 711

    Simu ya Mezani: +255 712264912

    Simu ya Mkononi: +255 712264912

    Barua Pepe: td@kondoatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Kondoa - Haki Zote Zimehifadhiwa