• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Kondoa Town Council
Kondoa Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Kondoa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Mipango ,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu sekondari
      • Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
      • Idara ya Usafi na Mazingira
      • Divisheni
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Miundombinu Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Viwanda Bishara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Usimamizi na Utawala wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugi na Uvuvi
    • Kitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Teknolojia,Habari,Mawasiliano na uhusiano
      • Kitengo cha Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wasimamizi wa vituo vya kupigia kura wafundwa

Tarehe iliyowekwa: October 25th, 2020

Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Kondoa Mjini Msoleni Dakawa amewataka wasimamizi wa vituo na wasimamizi wasaidizi wa vituo vya kupigia kura wakati wa uchaguzi mkuu kuzingatia maelekezo watakayopewa ili kuuvusha salama uchaguzi jimbo la Kondoa Mjini.

Kauli hiyo ameitoa wakati akifungua semina ya siku mbili ya wasimamizi hao inayofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Ualimu Bustani Kondoa Mjini.

"Kila mtu anajua kwanini ameteuliwa na mkumbuke mlioomba mlikuwa wengi ila nyie wachache mmeaminiwa kuwa mtalivusha salama taifa katika zoezi linalokuja mbele yenu na mjue kwasasa macho na masikio ya watu wote yapo majimboni msituangushe,"amesema Dakawa.

Aidha amewakumbusha kuwa uchaguzi upo wa mujibu wa sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali hivyo wakavizingatie kwani kwenda kinyume na hivyo watawajibika kwa mujibu wa sheria jambo ambalo si zuri kwao.

"Sitarajii kukutana na migogoro na mitafaruku kwenye vituo vya kupigia kura zaidi mkashirikiane kama timu moja kwani kila mmoja katika kituo ana majukumu yake,"amesisitiza Dakawa

Hata hivyo amewasihi wasimamizi hao kuepuka kuleta itikadi za vyama vyao kwa kuwa wameshakula kiapo cha kujitoa uanachama na wakumbuke kuwa wapo pale kama watumishi wa tume na serikali na si wanasiasa.

"Mkazingatie muda wa kufika kituoni, kituo kinafunguliwa saa 1:00 asubuhi na si muda wa wewe kufika kituoni na ujue kuchelewa kwako ni kuwakwamisha wananchi, na kubwa mkamtangulize Mungu katika kazi hii ili mmalize salama," amesema Dakawa

Akiongea kwa niaba ya wasimamizi wengine  Zainabu Shabani amewasihi washiriki wengine kwenda kuwa waaminifu katika kukamilisha zoezi hilo ili likamilike kwa amani na utulivu.

Semina hii imehudhuriwa na wasimamizi na wasimamizi wasaidizi zaidi ya mia 300 wa vituo vya kupigia kura jimbo la Kondoa Mjini na inafanyika kwa siku mbili ambapo imehudhuriwa pia na wasimamizi ngazi ya jimbo na kata.

Matangazo

  • Tangazo la mikopo inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu February 21, 2025
  • Matokeo ya kidato cha nne 2024 shule za Sekondari Kondoa Mji January 23, 2025
  • Tangazo la kushiriki mazoezi ya kila Jumamosi ya pili kila mwezi January 02, 2025
  • Tangazo la umilikishwaji viwanja January 02, 2025
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • SHULE BORA yawapatia mafunzo ya tathmini Walimu 66 wa Kondoa Mji

    May 26, 2025
  • "Vitengo vya Mawasiliano Serikalini viimarishwe"

    May 24, 2025
  • Maafisa Habari hakikisheni wananchi wanapata habari sahihi

    May 23, 2025
  • Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari la awali ngazi ya kata yatolewa kwa Watendaji Kondoa Mji

    May 14, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Matukio ya Mwenge wa Uhuru Kondoa Mji 2025
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mpango Mkakati
  • Maktaba ya Picha
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Sheria ndogo
  • Ripoti Mbalimbali
  • Fomu Mbalimbali
  • Miradi Inayoendelea

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Kwapakacha

    Anuani ya Posta: S.L.P 711

    Simu ya Mezani: +255 712264912

    Simu ya Mkononi: +255 712264912

    Barua Pepe: td@kondoatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Kondoa - Haki Zote Zimehifadhiwa