• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Kondoa Town Council
Kondoa Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Kondoa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Mipango ,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu sekondari
      • Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
      • Idara ya Usafi na Mazingira
      • Divisheni
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Miundombinu Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Viwanda Bishara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Usimamizi na Utawala wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugi na Uvuvi
    • Kitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Teknolojia,Habari,Mawasiliano na uhusiano
      • Kitengo cha Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wazazi, walezi wapewa wiki moja wanafunzi kidato cha kwanza 2020

Tarehe iliyowekwa: February 10th, 2020

Wazazi na walezi wa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2020 na hawajaripoti katika shule walizopangiwa wamepewa wiki moja kuhakikisha wanafunzi hao wanaripoti na kuanza masomo kabla ya kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Mhe. Sezaria Makota wakati wa kikao cha wadau wa Elimu kwa ajili ya kujadili mafanikio na changamoto za elimu katika Halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kondoa Irangi hivi karibuni.

“Wazazi iko shida kwenu mwanafunzi haendi shule na haumuulizi anapaswa kupigwa fimbo au mwanafunzi mtoro anakuja kumchongea mwalimu kwa mzazi badala yake mzazi anakuja juu kwa mwalimu hii si sawa tuache kulea watoto kama mayai tutawaharibu,”alisema Mhe. Sezaria.

Aidha aliwataka Maafisa Elimu Kata kufanyakazi zao kwa weredi kwani baadhi yao wameonekana wazembe kwa kutotimiza majukumu yao hivyo ili kufuta dhana hiyo ni jukumu lao kujituma katika nafasi zao na kuwasihi kuacha kuwapakazia ubaya Maafisa Elimu kwani wanafanya kazi zao vizuri na matokeo yanaonekana.

“Niwapongeze pia wakuu wa Shule ya Sekondari ya Kwapakacha na Shule ya Wasichana Kondoa kwa kujituma na kufanya kazi vizuri kwani matokeo yanaonekana ikiwa ni pamoja na Walimu Wakuu wa Mpalangwi, Kondoa Islamic na viongozi wa Wilaya na tukiendelea kushirikiana nina imani tutafikia malengo ya kupandisha elimu ya watoto wa Kondoa,”alisisitiza Mhe. Makota.

Akiongea katika kikao hicho Mwenyekiti wa Halmshauri ya Mji Wa Kondoa Mhe. Hamza Mafita alisema kuwa ili kuondokana na matatizo ya elimu katika Halmashauri ni kuanzisha Mfuko wa Elimu ambao utasaidia kupunguza changamoto zinazoikabili Elimu ambapo kila kata itapewa fedha kulingana na jinsi walivyochangia ili kutatua changamoto zinazowakabili.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kondoa aliwashukuru wadau kwa kujitokeza kwa wingi na kutoa mawazo chanya kwa lengo la kuboresha elimu ya mtoto wa Kondoa kwani maendeleo ya Kondoa yataletwa na wote walioshiriki kikao na wenye dhamana ya kuwahudumia wana Kondoa.

“Pamoja na yote kuanzia sasa ni marufuku Walimu Wakuu na Wakuu wa Shule kuitwa Wilayani mara kwa mara kwani kunawafanya washindwe kusimamia majukumu yao iwapo Idara ina maagizo wafuateni hukohuko mashuleni ikiwa ni pamoja na walimu wote na viongozi kufuata Sheria, Taratibu na Kanuni za utumishi wa Umma na kushirikiana na viongozi, wazazi na wanafunzi wote ili kuinua elimu,”aliongeza Mkurugenzi Dakawa.

Mmoja wa wadau kutoka Mtaa wa Hachwi ikiwa ni moja ya Shule zilizofanya vibaya Bw. Salim Bura alisema kuwa kwasasa wanajamii ya Hachwi wameamka na kuona umuhimu wa Elimu ambapo kwasasa wapo tayari kumpatia nyumba ya kuishi bila malipo Mwalimu atakayepangwa katika Shule Shikizi ya Kotumo na kuiomba Halmashauri kuwafikishia huduma muhimu ikiwemo maji na umeme.

Kikao cha wadau kimeketi ili kujadili mafanikio na changamoto za elimu katika Halmashauri ya Mji wa Kondoa na kilianza kwa kusoma taarifa za Idara za Elimu na maazimio ya vikao vya wadau wa Elimu katika ngazi ya kata na taarifa za Ofisi za Udhibithi Ubora wa Elimu, Chama Cha Walimu na Tume ya Watumishi wa Walimu na kilihudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani,wadau wa Elimu, Wakuu wa Shule, Walimu Wakuu, Maafisa Elimu Kata, viongozi wa dini na Wazee maarufu.

Matangazo

  • Tangazo la mikopo inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu February 21, 2025
  • Matokeo ya kidato cha nne 2024 shule za Sekondari Kondoa Mji January 23, 2025
  • Tangazo la kushiriki mazoezi ya kila Jumamosi ya pili kila mwezi January 02, 2025
  • Tangazo la umilikishwaji viwanja January 02, 2025
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • Mkurugenzi Majaliwa aagiza miradi kukamilika ifikapo Mei 31

    May 08, 2025
  • ALAT mkoa wa Dodoma yatembelea miradi ya maendeleo Kondoa Mji

    May 03, 2025
  • Baraza la Madiwani lajivunia mafanikio kipindi cha miaka mitano

    April 30, 2025
  • Baraza la kazi robo ya tatu lafanyika Kondoa Mji Ushirikiano ukisisitizwa

    April 29, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Matukio ya Mwenge wa Uhuru Kondoa Mji 2025
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mpango Mkakati
  • Maktaba ya Picha
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Sheria ndogo
  • Ripoti Mbalimbali
  • Fomu Mbalimbali
  • Miradi Inayoendelea

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Kwapakacha

    Anuani ya Posta: S.L.P 711

    Simu ya Mezani: +255 712264912

    Simu ya Mkononi: +255 712264912

    Barua Pepe: td@kondoatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Kondoa - Haki Zote Zimehifadhiwa