• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Kondoa Town Council
Kondoa Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Kondoa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Divisheni
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Utumishi na Utawala
      • Idara ya Mipango ,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu sekondari
      • Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
      • Idara ya Usafi na Mazingira
      • Divisheni
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Miundombinu Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Viwanda Bishara na Uwekezaji
      • Divisheni ya Usimamizi na Utawala wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Kilimo, Mifugi na Uvuvi
    • Kitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Teknolojia,Habari,Mawasiliano na uhusiano
      • Kitengo cha Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • UKIMWI
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za Shughuri za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CCM Dodoma wampongeza Rais kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum

Tarehe iliyowekwa: July 17th, 2024

Kamati ya siasa mkoa wa Dodoma wamempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali na kuwasaidia wenye mahitaji maalum ikiwemo kuwajengea mabweni mawili kwa ajili yao katika Shule ya Msingi Iboni iliyopo katika Halmashauri ya Mji Kondoa kata ya Chemchem.

Pongezi hizo zimetolewa na Katibu wa CCM mkoa wa Dodoma Ndg. Pili Agustino wakati wa ziara ya kutembelea mradi wa mabweni mawili yaliyojengwa katika shule hiyo hivi karibuni.

“Nakumbuka nilikuja hapa mwaka 2023 tulikuja hapa tulikuwa bado hatujaanza ujenzi tukaongea na kupokea changamoto za hawa watoto ambapo wengine walikuwa wanatembea umbali mrefu na wazazi wao walikuwa wanashindwa kuwaleta hapa kutokana na changamoto ya kipato walizonazo,”amesema Katibu Pili

Ameendelea kueleza kuwa kutokana na kuwa Mheshimiwa Rais ni msikivu na anawapenda watoto akasikia kilio chao na akawaletea fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili ya watoto wenye mahitaji maalum ambapo wanasoma makika mazingira mazuri na salama na kuondokana na hali ya awali ambapo walikuwa wanasoma katika mazingira magumu.  

Aidha amewataka walimu kuyatunza mabweni hayo na kuhakikisha wanafunzi wanayatumia vizuri ili wenzao watakaokuja waweze kuyatumia yakiwa katika hali nzuri na imara kwani watoto hao ni wenye mahitaji maalum na wanatakiwa walelewe vizuri na kuelekezwa kufanya vitu mbalimbali.

“Tuna imani shule hii itaendelea kuwapokea na watoto wengine kutoka mikoa na wilaya nyingine si Kondoa tu hivyo tunawakaribisha wazazi wenye watoto wenye mahitaji maalum kwani mabweni ni mazuri na salama na tuache tabia ya kuwaficha watoto ndani tuwalete shule kwani wanaweza kusoma na kufaulu vizuri na kupata kazi,”amesisitiza Katibu Pili

Akiongea kwa niaba ya wenzake mwanafunzi Rahma Ramadhani mwenye ulemavu wa macho amemshukuru Rais kwa kuwajengea mabweni na kumuombea ili apate fedha zaidi ambazo zitasaidia katika ununuzi wa vifaa vya kujifunzia shuleni hapo ambavyo vinakosekana shuleni hapo.

Akisoma awali taarifa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Iboni Mwalimu Charles Phabian amesema shule hiyo ilipokea fedha shilingi milioni 142 kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa ajili ya ujenzi wa bweni moja, vitanda na magodoro pamoja na shilingi milioni 128 kutoka serikali kuu kwaajili ya ujenzi wa bweni na vitanda vya wanafunzi wenye mahitaji maalum ambayo yote yamekamilika.

Mabweni yaliyojengwa katika Shule ya Msingi Iboni kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum yamekamilika ambapo Kamati ya Siasa mkoa imeshauri yaanze kutumika mapema mwezi Agosti na yatahudumia wanafunzi kutoka ndani nan je ya Kondoa na yana uwezo wa kubeba wanafunzi 200 wakike 120 na kiume 80 ambapo kwa sasa kuna jumla ya watoto 30 wenye mahitaji maalum kwenye shule hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la mikopo inayotolewa kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu February 21, 2025
  • Matokeo ya kidato cha nne 2024 shule za Sekondari Kondoa Mji January 23, 2025
  • Tangazo la kushiriki mazoezi ya kila Jumamosi ya pili kila mwezi January 02, 2025
  • Tangazo la umilikishwaji viwanja January 02, 2025
  • Tazama Vyote

Habari Mpya

  • Mkurugenzi Majaliwa aagiza miradi kukamilika ifikapo Mei 31

    May 08, 2025
  • ALAT mkoa wa Dodoma yatembelea miradi ya maendeleo Kondoa Mji

    May 03, 2025
  • Baraza la Madiwani lajivunia mafanikio kipindi cha miaka mitano

    April 30, 2025
  • Baraza la kazi robo ya tatu lafanyika Kondoa Mji Ushirikiano ukisisitizwa

    April 29, 2025
  • Tazama Vyote

Video

Matukio ya Mwenge wa Uhuru Kondoa Mji 2025
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Mpango Mkakati
  • Maktaba ya Picha
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Sheria ndogo
  • Ripoti Mbalimbali
  • Fomu Mbalimbali
  • Miradi Inayoendelea

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana nasi

    Mtaa wa Kwapakacha

    Anuani ya Posta: S.L.P 711

    Simu ya Mezani: +255 712264912

    Simu ya Mkononi: +255 712264912

    Barua Pepe: td@kondoatc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faraga
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Kondoa - Haki Zote Zimehifadhiwa